Rafiki yangu mpendwa karibu
Leo napenda kukukaribisha katika somo la leo ambalo kila mmoja wetu katika jamii linamfaa kulifaham
Sasa katika kupangilia bajeti kunamambo ya kuzingatia ambayo yatagawanyika katika sehem mbili sehem ya kwanza ni katika upangaji wa bajeti kwa mtu asie na madeni na mwenye madeni
Bajeti kwa mtu asie na madeni
Katika sehem hii ya kwanza mtu anapaswa kugawanya fedha zake katika sehem sehemu kama ifuatavyo
1:Asilimia 50 ya kipato
Hii ni nusu ya kipato chako ambayo unapaswa kuigawa kwanza ili ihusike na mambo ya muhimu na lazima kwa rugha nyepesi ni mambo ambayo huwezi kuishi kama ukiyakosa mfano chakula,maradhi, mavazi na mengineyo kulingana na levo ya maisha yako,,, hii haiusishi manunuzi ya bando, cheni, pombe au kitu chochote cha stalehe .
2: Asilimia 30 ya kipato chako
Katika sehem hii ya pili inahususha matumizi ya muhimu lakini sio ya lazima nikiwa namaanisha matumizi ambayo ukiyakosa unaweza kuishi vizur tu kulingana na daraja lako la kimaisha mfano manunuzi ya bando na mengineyo kulingana na levo ya maisha yako
3: Asilimia 20 ya kipato chako
Hii itahusika katika uwekezaji na akiba nikiwa na maana kwamba Asilimia 10 ni kwaajil ya uwekezaji na Asilimia 10 NYINGINE ni kwaajili ya akiba ,,,,kumbuka utajili haupimwi kwa kiasi unachoingiza bali unapimwa kulingana na kiasi unachobakiza
Kwa wenye madeni fatilia makara itakayo fata usisahau comment na like yako
Leave a comment